Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya YANGA

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 09, 2016

Picha

AL AHLY WAPASHA MARA YA MWISHO

Picha
MAZOEZI YA MWISHO YA AL AHLY TAIFA KABLA YA KUIVAA YANGA KESHO TAIFA MAZOEZI YA MWISHO YA KIKOSI CHA AL AHLY KABLA YA MECHI YA KESHO DHIDI YA YANGA KWENYE UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM. CHINI YA KOCHA MARTIN JOL, KIKOSI HICHO KILIFANYA MAZOEZI YAKE HAYO LEO HII JIONI KWENYE UWANJA HUO.

AL AHLY USO KWA USO NA YANGA TAIFA

Picha
Yanga watakutana na Al Ahly uwanja wa taifa Dar es Salaam Klabu ya Young Africans itashuka dimbani kesho Jumamosi kucheza dhidi ya miamba wa Misri Al Ahly hatua ya 16 bora katika Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL). Mechi hiyo itachezewa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuanzia saa 10 kamili kwa saa za Afrika Mashariki.

RATIBA LIGI KUU BARA

Picha
  Katika mwendelezo wa ligi kuu Tanzania bara leo watani wa jadi Simba na Yanga wanakutana katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ikiwa kila timu inakamilisha mechi yake ya nne tangu kuanza kwa ligi msimu huu wa 2015/16.Mechi hii inatarajiwa kuanza majira ya saa 10:00 jioni. Mechi nyingine za Ligi Kuu ya Vodacom leo zitakuwa ni kati ya Coastal Union dhidi ya Mwadui FC katika Uwanja wa Mkwakwani mijini Tanga, Prisons na Mgambo JKT Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, JKT Ruvu na Stand United Uwanja wa Karume, Dar es salaam, Mtibwa Sugar na Majimjaji ya Songea Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro na Kagera Sugar na Toto Africans Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo miwili, kati ya Azam FC na Mbeya City Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na African Sports na Ndanda FC Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

SIMBA VS YANGA HAPATOSHI TAIFA LEO

Picha
WATANI wa jadi, Simba na Yanga SC wote walirejea jana Dar es Salaam kutoka kwenye kambi zao Zanzibar kuelekea pambano lao la leo. Miamba hiyo inatarajiwa kumenyana leo jioni Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kuanzia Saa 10:00.

YANGA SC WAWEKA KAMBI KUJIANDAA NA WAGOSI WA KAYA

Picha
MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga SC jana wameingia kambini katika hoteli ya Valley View, Mtaa wa Kongo, Kariakoo, Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wao wa kwanza wa LIgi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union Jumapili.

YANGA SC WAIENDEA BAGAMOYO COASTAL UNION, PATACHIMBIKA TAIFA JUMAPILI

Picha
MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga SC Jumatano wataingia kambini katika hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani kwa maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom mwishoni mwa wiki.