MATOKEO MECHI ZA EUROPA
Mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi akipachika bao safi mbele ya mabeki wa Dortimund Michezo minne ya robo fainali ya michuano ya Europa ligi imechezwa katika viwanja vinne tofauti. Liverpool wakiwa ugenini nchini Ujerumani walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Borrusia Dortmund, Divock Origi aliwafungia Liverpool bao la kuongoza kabla ya beki wa Dortmund Mats Hummels kusawazisha.