MESSI AJIUZULU BAADA YA KICHAPO
Mshambulizi wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amestaafu kutoka soka ya kimataifa. Mchezaji huyo bora zaidi duniani alitangaza hatua hiyo baada ya kukosa penalti iliyoiwezesha Chile kuilaza Argentina katika fainali ya mchuano wa Copa America.