MANCHESTER UNITED YAMSAJILI MKHITARYAN
Klabu ya Manchester United imemnunua kiungo wa kati raia wa Armenia aliyekuwa anayechezea klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani, Henrikh Mkhitaryan. Mchezaji huyo wa umri wa miaka 27 amejiunga na United kwa bei ambayo haikufichuliwa.