MWINGEREZA SIMBA AKOMAA NA NGOZI
KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Muingereza, Dylan Kerr, amesema kwamba kikosi chake kimepanga kufanya vizuri katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambayo inatarajiwa kuanza Jumamosi kwa kupata ushindi wa 'kihistoria' ugenini itakapokabiliana na wenyeji African Sports kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini, Tanga.