WADUKUZI WA URUSI WAFICHUA FAILI ZAIDI ZA WADA
Wanariadha hao 
wanajumuisha muendeshaji baiskeli wa Uingereza Sir Bradley Wiggins, 
mwanariadha wa Olimpiki mwenye hadhi kubwa zaidi nchini humo, na bingwa 
mara nne wa mashindano ya Tour de France Chris Froome.
| Sir Bradley Wiggins ni miongoni mwa wanariadha ambaye taarifa ya kibinafsi ya matibabu imetolewa | 
Hakuna dalili zozote zinazowahusisha wanariadha hao na uhalifu.
Wada
 inasema kuwa udukuzi wa kimitandao ni jaribio la kudhoofisha mfumo 
mzima wa dunia wa kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli 
miongoni mwa wanariadha.
Mkurugenzi mkuu wa Wada Olivier Niggli, 
anakosoa ufujaji wa taaarifa hizo na kusema kwamba "hakuna shaka"  
udukuzi huo ulikuwa tendo la kulipiza kisasi dhidi ya ripoti ya Wada kwa
 wanariadha wa Urusi kwamba taifa hilo iliwasaidia wanariadha wake 
kudanganya huku akiomba utawala nchini Urusi kuzima udukuzi huo.
Rekodi
 hiyo ilitolewa na kundi moja linalojiita "Fancy Bears" mara nyingi 
ikishinikiza kile kinachojulikana kama  "Therapeutic Use Exemptions" 
(TUEs) na kukubalia dawa zilizopigwa marufuku kutumika na "wanariadha" 
ili kuthibitishwa mahitaji ya matibabu.
Kundi hilo linasema kuwa TUEs  "imeidhinishwa kutumika" na kwamba Wada  "ni fisadi na inaeneza udanganyifu".
Taarifa
 hiyo inahusisha Wamarekani 10, Waingereza 5 na Wajerumani 5 kwa pamoja 
na mwanaridha mmoja mmoja kutoka Denmark, Urusi, Poland, Romania na 
Jamhuri ya Czech.
Orodha hiyo pia 
inajumuisha majina 11 washindi wa medali mbali mbali katika mashindano 
ya mbio zilizomalizika hivi majuzi mjini Rio De Jeneiro, likiwemo jina 
la mmarekani Bethanie Mattek-Sands, ambaye alishinda dhahabu katika 
mashindano ya tennis inayojumuisha wachezaji wawili.
Ufujaji huu 
mpya unafuatia mwingine uliotokea hapo awali ambapo taarifa inayohusiana
 na wanariadha wa Marekani ilitolewa akiwemo mshindi wa dhahahu wa 
mazoezi ya viungo Simone Biles.
Maoni
Chapisha Maoni