WADUKUZI WA URUSI WAFICHUA FAILI ZAIDI ZA WADA

Simone Biles' pia ametajwa
Wadukuzi wanaoaminika kutoka Urusi wametoa faili zaidi ya wanariadha zilizoibwa kutoka kwa mamlaka kuu duniani ya kudhibiti utumiaji wa dawa za kusisimua misuli miongoni mwa wanariadha (Wada).
Wanariadha hao wanajumuisha muendeshaji baiskeli wa Uingereza Sir Bradley Wiggins, mwanariadha wa Olimpiki mwenye hadhi kubwa zaidi nchini humo, na bingwa mara nne wa mashindano ya Tour de France Chris Froome.
Sir Bradley Wiggins ni miongoni mwa wanariadha ambaye taarifa ya kibinafsi ya matibabu imetolewa
Sir Bradley Wiggins ni miongoni mwa wanariadha ambaye taarifa ya kibinafsi ya matibabu imetolewa
Hakuna dalili zozote zinazowahusisha wanariadha hao na uhalifu.
Wada inasema kuwa udukuzi wa kimitandao ni jaribio la kudhoofisha mfumo mzima wa dunia wa kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli miongoni mwa wanariadha.
Mkurugenzi mkuu wa Wada Olivier Niggli, anakosoa ufujaji wa taaarifa hizo na kusema kwamba "hakuna shaka" udukuzi huo ulikuwa tendo la kulipiza kisasi dhidi ya ripoti ya Wada kwa wanariadha wa Urusi kwamba taifa hilo iliwasaidia wanariadha wake kudanganya huku akiomba utawala nchini Urusi kuzima udukuzi huo.
Rekodi hiyo ilitolewa na kundi moja linalojiita "Fancy Bears" mara nyingi ikishinikiza kile kinachojulikana kama "Therapeutic Use Exemptions" (TUEs) na kukubalia dawa zilizopigwa marufuku kutumika na "wanariadha" ili kuthibitishwa mahitaji ya matibabu.
Kundi hilo linasema kuwa TUEs "imeidhinishwa kutumika" na kwamba Wada "ni fisadi na inaeneza udanganyifu".
Taarifa hiyo inahusisha Wamarekani 10, Waingereza 5 na Wajerumani 5 kwa pamoja na mwanaridha mmoja mmoja kutoka Denmark, Urusi, Poland, Romania na Jamhuri ya Czech.
Miongoni mwa majina hayo kutoka Jamhuri ya Czech ni bingwa mara mbili wa mchezo wa Tennis wa Wimbledon Petra Kvitova na mshindi wa medali ya dhahabu kwenye mashindano ya olimpiki ya London mwaka 2012, Robert Harting, raia wa Ujerumani.
Orodha hiyo pia inajumuisha majina 11 washindi wa medali mbali mbali katika mashindano ya mbio zilizomalizika hivi majuzi mjini Rio De Jeneiro, likiwemo jina la mmarekani Bethanie Mattek-Sands, ambaye alishinda dhahabu katika mashindano ya tennis inayojumuisha wachezaji wawili.
Ufujaji huu mpya unafuatia mwingine uliotokea hapo awali ambapo taarifa inayohusiana na wanariadha wa Marekani ilitolewa akiwemo mshindi wa dhahahu wa mazoezi ya viungo Simone Biles.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii