UFARANSA YAISAMBARATISHA ICELAND

 
Dimitri Payet akibusu kiatu cha Antonie Griezmann baada ya kufunga bao
 Ufaransa imefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali baada ya kuipa kichapo cha bao 5-2 timu ya Iceland hapo jana usiku.
Iceland wameondoka katika Euro lakini kwa hakika watabaki katika vinywa vya wapenzi wa Soka. Nahodha wao Aron Gunnarsson amesema kwa hakika huu ni mwanzo wao wa kuanza kukwea jukwaa la kimataifa.

Paul Pogba scores their second goal of the game with a header
Pogba akiifungia Ufaransa bao la pili
Anasema kile walichokipata jana katika Stade de France kimewasikitisha lakini wanajivunia ushiriki wao kwani umewajenga sana.
Dimitri Payet puts France 3-0 up
Payet akiifungia timu yake ya taifa bao la tatu
Sasa wanajipanga katika kuwania kufuzu kushiriki kwa mara ya kwanza katika kombe la Dunia litakalofanyika Urusi mwaka 2018 wakiwa kwenye kundi ambalo lina Croatia, Ukraine, Finland, Uturuki na Kosovo.
Olivier Giroud was substituted after scoring the second
Giroud  akishangilia goli lake la pili
Inakadiriwa asilimia 10 ya Raia wote wa nchi walikuwa wamesafiri kuja kuishabikia timu yao.
Michuano hii pia imetumika kuwatangaza wachezaji na sasa tutaanza kukona wakienda huku na kule, kwa mfano mshambuliaji Hal Robson Kanu wa Wales ambaye ameachwa huru na Reading mwishoni mwa msimu wa 2015-16 hivi sasa ameanza kutakiwa huku na kule na hasa baada ya bao lake lile alilogeuka katika kumi na nane akawabamiza ubelgiji na kuipeleka Wales nusu fainali.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii