MURRY NA SERENA WASONGA MBELE

Serena Williams na Andy Murray wamefanikiwa kutinga katika mzunguko wa pili wa michuano ya Wimbledon inayoendelea mjini London.

 Kwa upande wa Serena yeye amemchakaza Amra Sadikovic kwa seti 6-2,6-4 huku Murray akimchapa Liam Broady kwa seti 6-2 6-3 6-4 katika mchezo uliokuwa wa kukata na shoka.
 
Katika mzunguko wa pili Serena Williams atacheza dhidi ya Christina McHale huku Andy Murray mwenye miaka 29 akikipiga na Yen-Hsun Lu kutoka china.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii