MATOKEO EPL WEEKEND HII, LEICESTER HAISHIKIKI, MAN YAPIGWA 3

Jamie Vardy of Leicester City celebrates as he scores their first goal against Sunderland
Ligi kuu ya soka ya England imeendelea tena jumapili kwa michezo mitatu ,Sunderland wakicheza nyumbani dhidi ya vinara wa ligi Leicester city, waliambulia kipigo cha mabao 2-0, na kuwafanya leicester city kufikisha alama 72 katika Msimamo.Liverpool waliibamiza stoke city kwa kichapo cha mabao 4-1 yaliyofungwa na wachezaji Alberto Moreno, Daniel Sturridge na Divock Origi (mabao mawili) huku bao pekee la kufutia machozi la stoke city likifungwa na Bojan Krikic.
Liverpool's Divock Origi celebrates scoring his side's third goal of the game
Mchezaji wa Liverpool Divock Origi akishangilia mara baada ya kuifungia timu yake goli la tatu dhidi ya Stoke City hapo jana
Na Mechi ya tatu ya mwisho kati ya Tottenham na Manchester united mchezo ulimalizika kwa United kuchabangwa mabao 3-0.

Dakika ya 70 mchezaji Dele Alli alianza kuiptia goli bao la kwanza Tottenham .

Erik Lamela of Tottenham Hotspur celebrates as he scores their third goal
Erik Lamela wa Tottenham Hotspur akishangilia mara baada ya kuifungia timu yake goli la tatu
Tottenham iliandika bao la pili kupitia kwa Toby Alder-weireld, huku bao la tatu likipachikwa na Erick Lamela dakika ya 76.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii