HUYU PEDRO WA MOURINHO NI SHIDAAAA......!!

Ni kwa siku nyingi wachambuzi wengi walikuwa wakijiuliza ni yupi mchezaji ndani ya Chelsea ambaye ataweza kuwasumbua mabeki zaidi ya Hazard!! jibu walikuwa hawalipati lakini kwa sasa jibu limepatikana kuwa chaguo la Mourinho ni sahihi (Pedro)

Bila shaka kwa sasa mashabiki wa Chelsea wanauona umuhimu wa Pedro kuanzia kulinda hadi kushambulia, kitu hicho kilimchanganya sana Mourinho wakati wa mechi dhidi ya West brom ambapo wakati akifikilia kumpumuzisha ghafla Terry akapewa Kadi nyekundu hivyo ikamlazimu kumtoa Willian badala ya Pedro na kumuingiza cahil, hiyo ilionesha ni kwa kiasi gani alimwamini Pedro kuliko Willian kwa kushambulia na kurudi kukaba.
Ikiwa ni siku yake ya kwanza, Pedro alionesha kuelewana sana na Fabregas pamoja na Hazard ukiwa ni muda mfupi kweli waliokaa pamoja.
Hivyo mara baada ya kumalizika kwa mchezo Pedro alikuwa mchezaji bora wa siku na kupewa zawadi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii