BARCELONA YAPATA PIGO

Beki mashuhuri wa Barcelona Gerard Pique amefungiwa mechi nne baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi wa pembeni na kutolewa nje kwa kadi wakati wa mechi ya Kombe kuu la Hispania(Spanish Super Cup).

Pique mwenye umri wa miaka 28 amepewa adhabu hiyo kutokana na kosa alilolifanya siku ya juma tatu dhidi ya Athletic Bilbao mapema kipindi cha kwanza.
Mchezaji huyo wakimataifa wa Hispania ameonekana akiliongelea suala hili katika mtandao wake wa twitter huku akikanusha madai hayo ya kutumia lugha chafu.
Barcelona walilazimishwa sare ya 1-1 lakini wakazidiwa kwa uwiano wa magoli 5-1 kutokana na mechi ya kwanza.
Klabu hiyo bado haijaonesha kukata rufaa kutokana na kufungiwa kwa mchezaji huyo.
Barcelona jumapili wataanza ligi huku wakipambana tena na Bilbao katika La Liga, katika mpambano huo Pique ataukosa ikiwa ni pamoja na ule wa tar 2/9 dhidi ya Atletico Madrid.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii