DIAFRA SAKHO KUCHUNGUZWA NA FIFA


Mchezaji Diafra Sakho na kilabu ya West Ham zinakabiliwa na uchunguzi kutoka shirikisho la soka duniani FIFA kufuatia hatua ya mchezaji huyo kujiondoa katika
kikosi cha Senegal katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika.
FIFA inasema kuwa imefungua uchunguzi wa kinidhamu kwa kukiukwa kwa sheria.
Sakho 25,alijiondoa akiwa na jeraha la mgongo ,lakini baadaye akaifungia bao West Ham katika mechi yake ya FA dhidi ya Bristol City.
Sheria za FIFA zinasema kuwa mchezaji hawezi kuichezea kilabu yake iwapo anatakikana kuichezea timu yake ya taifa,lakini West Ham imekana kufanya makosa yoyote.

Sakho akishambulia kwa kasi

Sakho akishangilia baada ya kufunga bao 

Sakho na staili ya kuwabeza wapinzani
 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii