TANZANIA KWENDA OLIMPIKI-GOFU


Chama cha gofu nchini hapa kimetoa kalenda ya mwaka ya 2015 ya michezo ikionesha michuano mbalimbali ikiwemo ya Afrika ya Mashariki Kanda ya 5, ambayo itakuwa ni sehemu ya kufuzu kucheza Olimpiki mwakani mjini Rio de Janeiro, Brazil.


Kituo cha mchezo wa Golf kilichopo Arusha


Gofu na raga itakuwa ni sehemu ya michezo itakayoshindaniwa katika Olimpiki ya mwakani na TGU baada ya kuidhinishwa na kamati ya Olimpiki duniani (IOC) kama sehemu ya michezo itakayoshindaniwa.
Na kutokana na hilo, TGU imedhamiria kupeleka timu Brazil. Michuano hiyo ya kanda ya 5 ya Afrika itafanyika Kigali, Rwanda baadae mwaka huu.
Baadhi ya walimu wa mchezo wa golfu nchini

Kabla ya kwenda Kigali, TGU inategemewa kuandaa hafla ya kuchangisha fedha mwishoni mwa mwezi wa tatu mjini Arusha, kaskazini mwa Tanzania kwa ajili ya maandalizi ya timu ya taifa. 
 Timu ya mchezo wa golfu nchini ya mwaka 2013 wakiwa na walimu wao

Uchangishaji fedha pia utafanyika baade kati kati ya mwaka huu
Miongoni mwa michuano ya kimataifa ambayo Tanzania inategemewa kushiriki ni pamoja na michuano ya wazi ya Kenya (Kenya Open) na Coast Open itakayofanyika kati ya February na March, ambayo itakuwa ni kama sehemu ya maandalizi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii